Source : Habari leo
Posted by: Webmaster on 30-Jan-2010
MBUNGE wa Koani, Haroub Said Masoud, amewaonya wanaomtumia ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (SMS) za mapenzi.
Mbunge huyo ametangaza bungeni kuwa anampenda mke wake hivyo wanaomtumia SMS za mapenzi hawawezi kumyumbisha.
Masoud amewaonya kuwa wakifanya hivyo atatumia sheria mpya iliyopitishwa leo kuwashughulikia.
Kwa mujibu wa Mbunge huyo, SMS hizo zimewahi kusababisha mgogoro katika ndoa yake.
Amedai kuwa, kwa kuwa namba za wabunge zipo wazi,watu wasiofahamika wamekuwa wakiwatumia wabunge SMS za mapenzi.
Kwa mujibu wa Mbunge huyo, watu hao wakiwaona wabunge kwenye runinga, wanatafuta namba zao na kuwatumia SMS za mapenzi.
“Eti unapokea ujumbe unasema sweet I love you tuonane, kweli ujumbe kama huu mkeo akiuona atakuamini?” amehoji Mbunge huyo na kudai kuwa yeye ni miongoni mwa waathirika wa SMS za mapenzi.
| On 1st Feb,2010 Nyota wrote |
| Kujihami sio dhambi. |

